
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Maunda Zoro asema hivi karibuni ataanzisha Bendi yake mwenyewe. Akizungumza na Mwananchi Jumapili hivi karibuni, Maunda alisema; “Wazo la kuanzisha bendi nilipewa na kaka (Banana Zoro), lakini taratibu za kuanzisha bendi hiyo bado kidogo kukamilika. Alisema kuna baadhi ya vifaa havijakamilika, lakini anategemea hadi Aprili mwaka huu...