Monday, February 27, 2012
Friday, December 23, 2011
TANGAZO! TANGAZO! TANGAZO!
ASASI YA ACTION MUSIC TANZANIA (AMTZ) YENYE NAMBA YA USAJILI BST/4733 IMEANDAA NA ITAENDESHA MAFUNZO YA MUZIKI (NADHARIA NA VITENDO) KWA WATU WOTE KUANZIA TAREHE 09/01/2012 IDARA YA SANAA NA SANAA ZA MAONESHO (FPA) CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.
USAJILI UNAFANYIKA KATIKA OFISI ZETU (AMTZ) ZILIZOPO SHULE YA MSINGI MWENGE KARIBU NA MARYLAND BAR, KILA SIKU KUANZIA 20/12/2011 HADI 7/1/2012, SAA 4:00 HADI SAA 7:00 MCHANA, NA SAA 8:00 HADI SAA 11:00 JIONI. FOMU ZA USAJILI ZINAPATIKANA OFISINI KWA GHARAMA YA SHILINGI 3000/= TU
MAFUNZO YATAKAYOTOLEWA NI PAMOJA NA NADHARIA YA MUZIKI, UCHEZAJI/UPIGAJI WA ALA ZA MUZIKI ZIKIWEMO GITAA, KEYBOARD/PIANO, TARUMBETA, SAXOPHONE, KONGA, DRUM SET, NA UPIGAJI WA NGOMA ZA ASILI YA TANZANIA.
PIA YATATOLEWA MAFUNZO YA “BODY PERCUSSION” (Matumizi ya mwili kutengeneza midundo ya muziki)
KWA MAWASILIANO:-
+255 757 361 266
+255 716 515 853
+255 755 058 045
E-MAIL: actionmusictz@yahoo.com
www.actionmusictz.blogspot.com
Wednesday, September 21, 2011
MAFUNZO YA MUZIKI AGOSTI 2011, FPA, UDSM
Mwalimu wa muziki wa AMTZ Abeid Mussa akitoa maelekezo wakati mafunzo upande wa 'Music Ensemble'
Washiriki wa mafunzo ya muziki yaliyofanyika Agosti 8-21, 2011 wakifanya onyesho, katika kituo cha utamaduni cha Ujerumani, Goethe Institut-Tanzania kilichopo Upanga, Dar es Salaam
Thursday, August 18, 2011
| Invitation to a Concert |
| Saturday 20.08. 2011, Time: 19:30 - 20:40, Venue: Goethe-Institut |
| Action Music Tanzania Concert |
Action Music Tanzania has organized a concert to show the results of 14 days
music training for budding musician from Dar es Salaam, Pwani and Shinyanga.
The participants of the music training will perform a Nyamwezi melody,
a Makonde melody and a body percussion.
Goethe-Institut Tanzania
Alykhan Road No. 63 Time: 19.30 - 20.40
Date: 20.08.2011
|
Wednesday, August 10, 2011
MAFUNZO YA MUZIKI 10/08/2011
Mwalimu Geofrey Charahani akitoa maelekezo ya namna ya upigaji sahihi na wa kitaalamu wa vyombo vya kupiga (percussive instruments), Six ni miongoni mwa wanafunzi wanaoshiriki mafunzo ya muziki Agosti mwaka 2011.
Mwalimu Abeid Mussa na mwanafunzi wake wa gita
Mwalimu Damas Mpepo akitoa maelekezo kwa mwanafunzi wake wa chombo cha kupuliza mbinu muhimu katika kutumia chombo hicho.
Kwa mara ya kwanza Ishara ama Six akipiga drum baada ya kupewa maelekezo na mwalimu wake Geoffrey Charahani
Viongozi na walimu wa AMTZ wakiwa katika picha na baadhi ya wanafunzi wa mafunzo ya muziki
Viongozi na walimu wa AMTZ, waliosimama kutoka kulia ni Mratibu Damas Mpepo, Joyce Kirio, Katibu Mtendaji Mandolin Kahindi, Mweka Hazina Abeid Mussa, Mratibu Msaidizi Lazaro Kayombo, Suleiman Makame, Kauzeni Lyamba na Geoffrey Charahan, waliokaa ni baadhi ya wanafunzi walioshiriki mafunzo ya muziki.
Friday, March 25, 2011
Wednesday, March 23, 2011
AMTZ KUKUTANA WEEKEND HII
Na Dotto Kahindi
Walimu wa muziki Tanzania kutoka shirika la Action Music Tanzania wanakutana ijumaa hii katika chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa mafunzo ya muziki yatakayodumu kwa siku tatu.
Pamoja na mambo mengine walimu hao watajifua njia sahihi za kufundishia namna ya kuandika na kusoma muziki, mazoezi ya mnyumbuliko wa mwili na hamoni.
Tuesday, March 15, 2011
Monday, March 7, 2011
Saturday, February 26, 2011
Maunda Zoro kumiliki Bendi Tanzania
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Maunda Zoro asema hivi karibuni ataanzisha Bendi yake mwenyewe. Akizungumza na Mwananchi Jumapili hivi karibuni, Maunda alisema; “Wazo la kuanzisha bendi nilipewa na kaka (Banana Zoro), lakini taratibu za kuanzisha bendi hiyo bado kidogo kukamilika. Alisema kuna baadhi ya vifaa havijakamilika, lakini anategemea hadi Aprili mwaka huu atakuwa tayari ameshaianzisha ikiwamo kusajili bendi hiyo. “Jina la bendi bado sijalifikiria, ingawa nitawashirikisha baadhi ya wanamuziki wa Bongo fleva ambao sitawataja majina kwa sasa, kwani ni mapema mno,” alisema Maunda. Maunda alitamba na wimbo wa ‘Niwe wako’ na ‘Mapenzi ni ya wawili’ na ameshirikishwa kwenye nyimbo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Hellow wa Hussein Machozi na ‘Usinihukumu’ wa Steve.















.jpg)