Monday, July 16, 2012
BREAKING Newzz>>>CHEGE apata ajali mbaya ya gari usiku huu Temeke
Saturday, July 14, 2012
Afande Sele azijibu shutuma za 20 Percent
Uswahiba kati ya wasanii wawili wa Bongo Flava nchini,
Afande Sele na 20 Percent umeingia dosari baada ya kutupiana maneno kila mmoja
kwa nyakati tofauti kwenye vyombo vya habari.
Maneno hayo yalianza wiki iliyopita baada ya Afande Sele
kuzungumza na Clouds FM na kudai kusikitishwa na kitendo cha swahiba wake 20
Percent cha kugoma kutumbuiza kwenye tuzo za muziki za Zanzibar wakati alikuwa
amelipwa pesa zote.
Kufuatia mgomo huo, waandaaji walimpeleka lock-up msanii
huyo na kubaki na laptop yake mpaka pale atakapowarudishia waandaji hao
shilingi milioni moja waliyompa kwaajili ya kuperform kwenye tuzo hizo.
Hatimaye jana 20 Percent alizungumza na kituo hicho cha radio
kuhusiana na tukio lenyewe na kusema kuwa Afande Sele amechanganyikiwa na
anasumbuliwa na njaa ndio maana anamlaumu.
Akiongea kwa jaziba, 20 Percent amesema Afande Sele ni
kama ‘mtoto’ na alimshangaa kufahamu kuwa alifika Zanzibar saa sita usiku bila
kuwa sehemu ya kulala kutokana na waandaaji hao kuwa wababaishaji.
Leo (July 14) Afande Sele ametoa maelezo marefu
kuhusiana na sakata hilo kupitia Facebook. Hivi ndivyo alivyoandika:
“Salaam Ndugu zangu wote mashabiki na wadau wa muziki
wetu!!
Tamko langu kuhusiana na lugha zilizotolewa na Twenty
Percent kuhusiana na show yetu ya Zanzibar Music Award.
Tulialikwa kwenye ZANZIBAR MUSIC AWARD, na kabla ya kazi
makubaliano yote ya kazi kwa mujibu wa mkataba yalifuatwa, makubaliano hayo
yalihusisha sisi kujigharamia gharama zote za nauli na Malazi (accomodation).
Tulifika Zanzibar salama, tulipokua Zanzibar twenty
alitaka agharamiwe huduma zote ambazo ni nje ya mkataba wetu, nikamuomba na
kumsihi sana ndugu yangu aheshimu mkataba, asitafute matatizo kwani tayari
mpaka wakati huu tuna kesi na Halmashauri ya Manispaa ya Moro ambayo kimsingi
sikuhusika (nilishatolea ufafanuzi siku za nyuma).
Lakini yeye alipingana na mimi, akanibishia na
kunisukuma Mbele ya wageni na wenyeji wetu, wakiwemo Makamu wa pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seiph Ali Idi, Waziri Seiph Khatibu.
Walikuwepo waadishi wa habari wa siku Nyingi Akiwemo
Abubakari Liongo (idhaa ya kiswahili radio Ujerumani), Mkurugenzi wa ZENJI FM
ndugu Tua Saidi Tua.
Mimi Selemani Abdallah Juma Msindi sihusiki kwa namna
yoyote, na tabia zisizo za kuridhisha zinazoonyeshwa na Ndugu yangu Twenty
Percent, ambae nimekua nae nyumbani kwangu hata kabla ya Tuzo zake Tano (Kili
Music Award) ambazo kazi hizo zote hizo kaandikia nyumbani kwangu siwezi kuwa
na tatizo nae ni ndugu yangu kiimani na kikazi, hata kazi yangu niliyofanya nae
kabla siku za nyuma "MBELE YAKO NYUMA YANGU" .. Kuna mstari Nilisema
" ..Kuandika Rhyme kwenda Gym kimtindo kuonyesha Ugumu, bado unatakiwa uwe
na nidhamu ya kweli, sio ya kumzuga Mwalimu, utajihukumu".
Nimekua nikisisitiza nidhamu kwa Ndugu zangu woote toka
enzi za Ghetto BoyZ, Watupori na Mabwasha'Kingdom, ambao wengine hawafanyi
sanaa, ila nipo nao kwenye Familia yetu kubwa hapa Tanzania. Nimesikitishwa na
kitendo hicho. Siku zote nimekua mwenye kuhitaji suluhu kwa namna ya Amani.
Verry sorry kwa wote ambao mmefadhaika kwa hilo.
Tuendelee kuwa pamoja na msisite kutoa ushauri wenu, maoni ili Game letu
lisonge. MUNGU ATUBARIKI.
Asanteni sana.
Selemani Juma Abdallah Mutabhazi Msindi.
a.k.a Afande Sele (King of Rhymes)Chanzo: Leotainment blog
MAFANIKIO YA CHAMELEONE KATIKA MAISHA
Baada ya kukutana na staa wa
muziki kutoka Uganda Jose Chameleone nimegundua kuna mambo mengi nilikua
nayasikia tofauti na kuyasoma ambayo yeye ameyazungumza tofauti kabisa.
Nilikua sijui, kumbe Chameleone alianza kuenjoy kuwa staa kuanzia mwaka 2000 japo alianza muziki 1995, 2003/2004 ndio alianza kupata pesa na hapo ndipo maajabu yalianza kutokea kwa kuanza kutimiza ndoto.
Chameleone amesema “nilijenga nyumba yangu kwa miaka miwili ambapo 2005 ilimalizika na ikawa imegharimu shilingi milioni 200 -300 za kitanzania, wakati nilikua naijenga hiyo ndio pesa niliyokua nayo na nikasema kabla sijaipoteza acha nifanye kitu muhimu lakini Mungu akanibariki tena baada ya kujenga hiyo nyumba nikapata bahati nyingine nikaendelea na vitu vingine”
Exclusive na millardayo.com Mwimbaji huyu staa kutoka Uganda amesema vyanzo vyake vikubwa vya mapato kwa sasa ni kununua na kuuza ardhi, kuuza simu za mkononi ziitwazo Chameleone anazozitengeza China, kununua nyumba na kuziuza pia kupangisha nyumba.
kuhusu vyanzo vingine vya mapato Chameleone amesema “show pia zinatulipa sana Uganda japo siwezi kukwambia nalipwa bei gani kwa sababu sipendi kuonekana mtu wa kujisifia lakini kwa wiki moja naweza kupiga show mbili Kampala au Uganda, na kingine kinachotulipa sana ni Kampuni kubwa za biashara ambazo zikikuona una nguvu zinakuchukua na kukulipa vizuri kwa kufanya nao promoshen au mambo mengine ya mkataba wa biashara”
Hii ni kwa Hissani ya www.millardayo.com
Nilikua sijui, kumbe Chameleone alianza kuenjoy kuwa staa kuanzia mwaka 2000 japo alianza muziki 1995, 2003/2004 ndio alianza kupata pesa na hapo ndipo maajabu yalianza kutokea kwa kuanza kutimiza ndoto.
Chameleone amesema “nilijenga nyumba yangu kwa miaka miwili ambapo 2005 ilimalizika na ikawa imegharimu shilingi milioni 200 -300 za kitanzania, wakati nilikua naijenga hiyo ndio pesa niliyokua nayo na nikasema kabla sijaipoteza acha nifanye kitu muhimu lakini Mungu akanibariki tena baada ya kujenga hiyo nyumba nikapata bahati nyingine nikaendelea na vitu vingine”
Exclusive na millardayo.com Mwimbaji huyu staa kutoka Uganda amesema vyanzo vyake vikubwa vya mapato kwa sasa ni kununua na kuuza ardhi, kuuza simu za mkononi ziitwazo Chameleone anazozitengeza China, kununua nyumba na kuziuza pia kupangisha nyumba.
kuhusu vyanzo vingine vya mapato Chameleone amesema “show pia zinatulipa sana Uganda japo siwezi kukwambia nalipwa bei gani kwa sababu sipendi kuonekana mtu wa kujisifia lakini kwa wiki moja naweza kupiga show mbili Kampala au Uganda, na kingine kinachotulipa sana ni Kampuni kubwa za biashara ambazo zikikuona una nguvu zinakuchukua na kukulipa vizuri kwa kufanya nao promoshen au mambo mengine ya mkataba wa biashara”
Hii ni kwa Hissani ya www.millardayo.com
Friday, July 13, 2012
Tuesday, July 3, 2012
MAFUNZO YA KUPIGA ALA ZA MUZIKI
ACTION
MUSIC TANZANIA (AMTZ) YENYE NAMBA YA USAJILI BST/4733 ITATOA MAFUNZO YA UPIGAJI
WA ALA MBALIMBALI ZA MUZIKI (KWA VITENDO) KWA WATU WOTE
MAFUNZO YATAANZA:
TAREHE 16/07/2012
MAHALI: IDARA YA SANAA
NA SANAA ZA MAONESHO (FPA) CHUO
KIKUU CHA DAR ES SALAAM (SEHEMU YA MLIMANI)
KIKUU CHA DAR ES SALAAM (SEHEMU YA MLIMANI)
NJOO UJIFUNZE MBINU ZA KITAALAMU ZA KUPIGA/KUCHEZA GITAA, KEYBOARD/PIANO, TARUMBETA, SAXOPHONE, KONGA, DRUM
SET, NA UPIGAJI WA NGOMA ZA ASILI YA TANZANIA, BILA KUSAHAU MAFUNZO MAALUMU YA “BODY
PERCUSSION” (Matumizi ya mwili kutengeneza midundo ya muziki) NA USOMAJI WA “NOTATION” YATAKAOTOLEWA NA WATAALAM
WALIOBOBEA KATIKA TASNIA YA MUZIKI KUTOKA VYUO MBALIMBALI.
USAJILI UNAFANYIKA: IDARA YA SANAA NA SANAA ZA
MAONESHO (FPA) CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (MLIMANI)
FOMU
ZA USAJILI ZINAPATIKANA
FPA
SAA 4:00 ASUBUHI HADI SAA 10:00 JIONI KWA GHARAMA YA SHILINGI 3000/= TU. WAHI,
NAFASI NI CHACHE.
KWA
MAWASILIANO: +255 757 361 266
+255
714 553 239
+255
755 058 045
E-mail:
actionmusictz@yahoo.com/mandolintz@yahoo.co.uk/mpepodamas@gmail.com
www.actionmusictz.blogspot.com
NYOTE MNAKARIBISHWA
Saturday, June 30, 2012
Exclusive uchambuzi: Wazazi wa Dogo Janja fuatilieni maendeleo yake, msiwaachie Mapromota

Dogo Janja
Na Dotto Kahindi-Thisday Magazine, Blog za mikoa
Mwezi
Juni mwaka huu umekuwa ni mwezi wa huzuni na furaha kwa nyota wa muziki
wa Bongo Fleva , Abdul Abubakar Chande ‘Dogo Janja’ kufuatia kutimuliwa
na Baba yake kimziki Madee na baada ya siku chache kurejea Dar es
Salaam na kuingia mkataba mpya na kampuni ya Mtanashati Entertainments.
Dogo
Janja alitimuliwa na Madee na kurejeshwa kwao jijini Arusha kwa madai
ya kushindwa kuzingatia masomo kwa kuendekeza utoro shuleni, kukosa
mwenendo mwema kimaadili sababu ambazo hata hivyo Dogo Janja
alizikanusha na kudai kuwa alikuwa akinyanyaswa na Madee.
Alidai
kuwa akiwa chini ya usimamizi wa Madee alikuwa akilipwa posho kidogo
baada ya kufanya maonyesho na kwamba Madee alihusika kumwibia pesa zake
benki hali iliyomfanya kuwa na salio la Tsh.25, 000 elfu tu katika
akaunti yake.
Hali
ilikuwa hivyo na imeleta picha mbaya na kuibua maswali mengi kwa
mashabiki wa muziki lakini lawama kubwa zinafaa kupelekwa kwa wazazi wa
Dogo Janja ambao walimruhusu kwa moyo mweupe aje kuishi na watu ambao
leo hii wanaonekana kuwa ni wahuni.
Pamoja
na kutimuliwa na Madee lakini sasa sasa amerejea tena akiwa katika
mwonekano mwingine, naamini muda mfupi aliokaa na wazazi wake walifanya
mazungumzo ya kutosha na kufanya makubaliano ya nini kipewe kipaumbela
katika maisha yake kwa sasa, ili kumjengea mafanikio yake kielimu na
kimaisha pia.
Furaha
aliyoipata baada ya kutua Bongo na kujiunga na kampuni ya Mtanashati
Entertainments ya jijini Dar es Salaam, zisimfanye akajisahau tena na
kuendeleza upuuzi alioufanya akiwa na Madee.
Tukubaliane
wote kuwa Dogo Janja bado ni mtoto na anahitaji kupata mwongozo wa
kutosha kutoka hasa kwa wazazi wake na watu walio juu ya uwezo wake ili
kumsaidia kufanya kila hatua kwa usahihi asije kujuta baadaye.
Pengine
kwa hatua ya nyota huyo cha kwenda kusomewa kisomo maalumu cha kuomba
Mwenyezi Mungu amnyooshee mambo yake pindi atakapoanza kushusha ngoma
mpya kinaweza kuonyesha kuwa kuna nia njema kwa watu alionao sasa.
Maneno
ya Mkurugenzi wa kampuni hiyo Ostaz Juma na Musoma kuwa wameamua
kumfanyia kisomo hicho kwa lengo la kuweka kazi zote za Dogo janja
mikononi mwa Mungu ili kumkinga na watu wabaya ambao kwa namna moja ama
nyingine hawajafurahishwa na mpango mzima wa dogo huyo kurejea Bongo.
Hata
hivyo katika kipindi kifupi alichojiunga na kampuni hiyo Dogo janja
amefanyiwa ‘shopingi’ ya nguvu kwenye maduka makubwa ya viwalo yaliyopo
Mlimani City jijini Dar ambayo ilitumia zaidi ya shilingi Milioni 2.5.
Hivi
ni miongoni mwa vitu vinavyomfanya Dogo Janja afurahie kuwa katika
kampuni hiyo lakini lazima ajue kuwa nidhamu ya kazi ndiyo itamfanya
aendelee kupata matunda hayo maana akiendelea kujifanya nunda na kupuuza
ya wakubwa wake haitamsaidia.
Monday, February 27, 2012
Friday, December 23, 2011
TANGAZO! TANGAZO! TANGAZO!
ASASI YA ACTION MUSIC TANZANIA (AMTZ) YENYE NAMBA YA USAJILI BST/4733 IMEANDAA NA ITAENDESHA MAFUNZO YA MUZIKI (NADHARIA NA VITENDO) KWA WATU WOTE KUANZIA TAREHE 09/01/2012 IDARA YA SANAA NA SANAA ZA MAONESHO (FPA) CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.
USAJILI UNAFANYIKA KATIKA OFISI ZETU (AMTZ) ZILIZOPO SHULE YA MSINGI MWENGE KARIBU NA MARYLAND BAR, KILA SIKU KUANZIA 20/12/2011 HADI 7/1/2012, SAA 4:00 HADI SAA 7:00 MCHANA, NA SAA 8:00 HADI SAA 11:00 JIONI. FOMU ZA USAJILI ZINAPATIKANA OFISINI KWA GHARAMA YA SHILINGI 3000/= TU
MAFUNZO YATAKAYOTOLEWA NI PAMOJA NA NADHARIA YA MUZIKI, UCHEZAJI/UPIGAJI WA ALA ZA MUZIKI ZIKIWEMO GITAA, KEYBOARD/PIANO, TARUMBETA, SAXOPHONE, KONGA, DRUM SET, NA UPIGAJI WA NGOMA ZA ASILI YA TANZANIA.
PIA YATATOLEWA MAFUNZO YA “BODY PERCUSSION” (Matumizi ya mwili kutengeneza midundo ya muziki)
KWA MAWASILIANO:-
+255 757 361 266
+255 716 515 853
+255 755 058 045
E-MAIL: actionmusictz@yahoo.com
www.actionmusictz.blogspot.com
Wednesday, September 21, 2011
MAFUNZO YA MUZIKI AGOSTI 2011, FPA, UDSM
Mwalimu wa muziki wa AMTZ Abeid Mussa akitoa maelekezo wakati mafunzo upande wa 'Music Ensemble'
Washiriki wa mafunzo ya muziki yaliyofanyika Agosti 8-21, 2011 wakifanya onyesho, katika kituo cha utamaduni cha Ujerumani, Goethe Institut-Tanzania kilichopo Upanga, Dar es Salaam
Thursday, August 18, 2011
| Invitation to a Concert |
| Saturday 20.08. 2011, Time: 19:30 - 20:40, Venue: Goethe-Institut |
| Action Music Tanzania Concert |
Action Music Tanzania has organized a concert to show the results of 14 days
music training for budding musician from Dar es Salaam, Pwani and Shinyanga.
The participants of the music training will perform a Nyamwezi melody,
a Makonde melody and a body percussion.
Goethe-Institut Tanzania
Alykhan Road No. 63 Time: 19.30 - 20.40
Date: 20.08.2011
|
Wednesday, August 10, 2011
MAFUNZO YA MUZIKI 10/08/2011
Mwalimu Geofrey Charahani akitoa maelekezo ya namna ya upigaji sahihi na wa kitaalamu wa vyombo vya kupiga (percussive instruments), Six ni miongoni mwa wanafunzi wanaoshiriki mafunzo ya muziki Agosti mwaka 2011.
Mwalimu Abeid Mussa na mwanafunzi wake wa gita
Mwalimu Damas Mpepo akitoa maelekezo kwa mwanafunzi wake wa chombo cha kupuliza mbinu muhimu katika kutumia chombo hicho.
Kwa mara ya kwanza Ishara ama Six akipiga drum baada ya kupewa maelekezo na mwalimu wake Geoffrey Charahani
Viongozi na walimu wa AMTZ wakiwa katika picha na baadhi ya wanafunzi wa mafunzo ya muziki
Viongozi na walimu wa AMTZ, waliosimama kutoka kulia ni Mratibu Damas Mpepo, Joyce Kirio, Katibu Mtendaji Mandolin Kahindi, Mweka Hazina Abeid Mussa, Mratibu Msaidizi Lazaro Kayombo, Suleiman Makame, Kauzeni Lyamba na Geoffrey Charahan, waliokaa ni baadhi ya wanafunzi walioshiriki mafunzo ya muziki.
















.jpg)