Tuesday, May 14, 2013

GOETHE INSTITUT-TANZANIA INVITE YOU TO AN OPEN STAGE NIGHT




On our OPEN STAGE NIGHT we invite you to perform. Whatever your talents might be, everyone is welcome to show them on stage. Please register now by sending us an e-mail or call us.E-mail: intern@daressalaam.goethe.org, Tel.:  075 375 152 and Tell us what you are planning to perform and the required technical equipment. 

Musicians can also bring their own instruments. entrance is fees.




Monday, May 13, 2013

USAJILI WA TUZO ZA MUZIKI ZA RFI WAANZA, WANAMUZIKI TANZANIA CHANGAMKIENI FURSA HII


Kwa usajili wa tuzo za muziki za rfi ambazo hufanyika kila mwaka na kuwashirikisha wanamuziki mbalimbali katika bara la Afrika bonyeza hapo chini rfi music award registration

Friday, May 10, 2013

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA SEMINA YA SOKO LA MUZIKI AFRIKA MASHARIKI 'DOADOA' JINJA UGANDA


 Washiriki katika semina ya kujadili changamoto za soko la muziki Afrika Mashariki wakifuatilia moja ya mada kwenye hotel ya Crasted Crane mjini Jinja, Uganda
 Mwanmuziki kutoka Kenya, Winyo akitumbuiza katika moja ya matamasha yanayoambatana na semina ya kujadili changamoto katika soko la muziki Afrika Mashariki.
 Wanamuziki wakiimba wimbo wa ushirikiano katika moja ya matamasha yanayoambatana na semina ya kujadili changamoto katika soko la muziki Afrika Mashariki, kutoka kushoto ni Mani Martin kutoka Rwanda, Shamsila kutoka Arusha Tanzania na Staffi kutoka Uingereza.


Kwa picha za matukio zaidi tembelea DOADOA 2013

Wednesday, May 8, 2013

SEMINA YA KUJADILI CHANGAMOTO ZA SOKO LA MUZIKI AFRIKA MASHARIKI 'DOADOA' YAFANYIKA UGANDA

Waendesha mada katika semina ya kuangalia changamoto katika soko la muziki Afrika Mashariki na njia za kuzitatua wakijadili umuhimu wa elimu ya muziki katika soko la muziki, kutoka kulia ni Katibu Mtendaji wa Action Music Tanzania, Mandoli Kahindi, Mkurugenzi wa sanaa kutoka Global Music Academy Ujerumani,William Ramsay, Muaandaaji wa muziki wa Uganda, Kazi Kasozi na Mkurugenzi Mtendaji wa Ketebul Music Kenya, Tabu Osusa


Semina hiyo ambayo inaambatana na maonyesho ya kazi mbalimbali za muziki yameandaliwa na Bayimba Cultural Foundation ya Uganda ambapo wadau mbalimbali wa muziki kutoka nchi mbalimbali wamejumuika kujadili na kubadilishana uzeofu juu ya soko la muziki kwa nchi za Afrika Mashariki. picha za matukio zaidi tembelea DOADOA

Wednesday, November 21, 2012

Exclusive Photos: Behind the scenes ya video mpya ya Makamua – Bado Kujuana

makamu (600x338)
makamua1 (600x338)
makamua3 (600x338)
makamua4 (600x338)
makamua5 (600x338)
makamua7 (600x338)
Love scene ilianzia hapa
Dr Eddo akitazama kitu
MMhhh
hapa nisaidie wewe
Dr Edooo
how deep is your love for me
Makamua akiwa amezungukwa na warembo

Makamua ametoa picha exclusive za behind the scenes ya video yake mpya inayotarajiwa kutoka rasmi leo. Picha hizi ni za wimbo wake mpya “Bado Kujuana” ambayo amemshirikisha msanii mwenzake Dr Eddo ambaye ndiye aliyefanya production zote mbili za audio na video ambapo picha zote za video zimechukuliwa jijini Mwanza.

Video : King Zilla ft Marco Chall – Nataka


SKYLIGHT BAND YAZIDI KUCHENGUA MASHABIKI @ THAI VILLAGE - MASAKI JIJINI DAR.

Pichani Juu na Chini Mashabiki wa SKYLIGHT BAND wakisakata mduara kwa raha zao katika ukumbi wa Thai Village jijini Dar es salaam.

Sunday, November 18, 2012

JB Mpiana kufanya Onyesho Dar Novemba 30

Mkurugenzi wa QS Muhonda J Entertainment, Joseph Muhonda (katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) katika ukumbi wa Millennium Business Park, Kijitonyama jijini Dar es Salaam mapema leo asubuhi wakati akizungumzia onyesho la Mwanamuziki wa Kimataifa kutoka nchini Congo,JB Mpiana kwa kushirikiana na Mashujaa Band litakalofanyika katika viwanja vya Leaders Novemba 30. Wengine kulia ni rais wa Mashujaa, Chaz Baba na kushoto ni Mshauri wa bendi, King Dodo.

Rose Muhando Kutikisa Tamasha la Shangwe Kagera

MWIMBAJI maarufu wa muziki  wa Injili nchini, Rose Muhando na mwenzake Enock Jonas (Zunguka) wanatarajiwa kutia chachandu katika tamasha la kwanza kubwa kufanyika Mkoani Kagera.
Tamasha hilo la Shangwe Kagera lina lengo la kuielimisha jamii na kuamsha mwamko wa kusaidia watoto yatima na wanaoishi katika maisha magumu.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Beula Communications Ltd, ambao ni waandaji wa tamasha hilo,Melkizedeck Mutta anasema kuwa matayarisho ya tamasha hilo yanaendelea vizuri kutokana na mwitikio mkubwa wa watu mbalimbali waliojitokeza kushiriki.
Pia, Mutta anasema bendi ya muziki ya wazawa mkoa huo, Kakau Band pamoja na vikundi vingine vya wanakwaya  wa makanisa mbalimbali, kikundi cha watoto yatima wanatarajia pia kutumbuiza.
Mutta anasema tamasha hilo la aina yake  linatajiwa kufanyika  Uwanja wa Kaitaba na pia kwenye ukumbi wa Lina’s mjini Bukoba, siku ya Uhuru, Desemba 9.
“Mpaka sasa tumekamilisha sehemu kubwa ya matayarisho hayo ikiwamo kulipia  uwanja pamoja sehemu ya malipo kwa wasanii ambao watashiriki,” alisema.
Pia, mkurugenzi huyo aliwaomba wadhamini zaidi na wadau wengine wa maendeleo na watoto kujitokeza kushiriki ili kuwasaidia jamii hasa watoto yatima na wengine wanaoishi katika mazingira magumu.
 Ni kuhamasisha jamii kuishi kwa amani,kupendana na kusaidia watu wengine hasa wasiojiweza kimaisha  ili na wao wajione ni sehemu yao.
Katika  kutambua hilo kampuni yetu iliamua kufanya utafiti mdogo nakugundua changamoto nyingi katika Mkoa wa Kagera, mojawapo ni kuwa na  watoto wengi wanaoishi katika mazingira magumu. Baada ya kuliona hili, tulitembelea vituo mbalimbali vya kulelea watoto hao, mojawapo ni Tumaini Children’s Centre   kinachomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Ki lutheri Tanzania (KKKT).
Kituo hiki kinalea watoto wote bila kujali kabila,jinsia wala dini zao,  kwa sasa kituo hiki kinahudumia watoto zaidi ya 800, kwa kuwapatia elimu,chakula, malazi n.k  ambapo kwa muda mrefu kimekuwa kikipata msaada toka Sweden ambao kwa sasa wametangaza kuusitisha kwa maelezo kuwa jamii ya Watanzania inapaswa kujifunza na kuanza kuhudumia watu wao wenyewe.
Kutokana na hilo ndiyo maana tumeonelea tuwe na tamasha la kuamasisha jamii ili ianze kuona umuhimu wa kusaidia  wenzao wanaohitaji msaada.

Saturday, November 17, 2012

Alliance Francois na onesho la utamaduni

na Khadija Kalili.
KITUO cha Utamaduni cha Ufaransa ‘Alliance Francois’ kimeandaa onesho la bure la muziki wa utamaduni wa Mwafrika katika kituo chake kilichoko Barabara ya Ali Hassan Mwinyi, jijini Dar es Salaam leo jioni.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa kituo hicho, Michael Shuma, aliwataja wasanii watakaonogesha onesho la leo kuwa ni Maryse Ngalula kutoka Kinshansa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Elie Kamano ‘General Kamano’ wa Guinea, ambaye anapiga muziki wake katika miondoko ya Hip Hop.
Alisema katika tamasha hilo, wasanii hao wawili watatumbuiza mmoja mmoja na baadaye watatoa burudani kwa pamoja.
Koshuma aliongeza kwamba, kituo hicho kimekuwa na utaratibu wa kufanya maonesho ya utamaduni mara kwa mara, na wanawashukuru wadhamini wao Shirika la Ndege la Precision kwa kutoa usafiri kwa wasanii hao, ambao mara baada ya onesho la Dar es Salaam watakwenda Arusha Jumapili, kisha Kilwa ambako nako watafanya maonesho.
Chanzo: Tanzania Daima

Friday, November 16, 2012

Busara Promotions yaanda shindano la waandishi wa makala za mtandaoni na magazetini

Wandaaji wa tamasha la kila mwaka la Sauti za Busara, Busara Promotions wameandaa shindano la uandishi wa makala mbalimbali kuhusiana na tamasha hilo zitakazochapishwa mtandaoni na kwenye magazeti na washindi kuzawadiwa zawadi mbalimbali.
Katika taarifa yake kwa waandishi wa habari, Busara Promotions imeandika:
Hii ni stori kwa ajili ya waandishi, wachapishaji na wenye mitandao ya kijamii. Kitu pekee katika tamasha la kumi la Sauti za Busara ambalo litaanza tarehe 14- 17 Februari 2013. Tamasha limefikia muongo mmoja ambalo hakuna mfano wake. Waandishi wanaombwa kutuma makala mitandaoni, blog na wachapishaji wa magazeti.
Mbali na kushapisha na kuweka makala mbalimbali, makala bora na mwandishi/mtunzi bora atazawadiwa fulana ya tamasha, pasi ya bure ya siku zote za tamasha na Posho kama ishara ya shukrani. Tuma kupitia barua pepe hii press@busara.or.tz mwisho tarehe 30/11/2012.
Tunasubiria kupokea makala bora. Tutawapa idhini waandishi bora kuendelea kuweka makala zao, chapisho mbalimbali kwenye blogs na tovuti baada ya tarehe ya mwisho. Makala bora itajadiliwa kutokana na uhalisia, mtazamo na idadi ya mitazamo/maoni kutoka kwa wasomaji na mashabiki.
Kuhusu Sauti za Busara
Sauti za Busara hufanyika kila mwezi wa pili katika kisiwa cha marashi ya karafuu Zanzibar, tamasha hujulikana kama ‘Tamasha rafiki katika sayari ya Dunia’. Katika kuwawezesha wenyeji ili wafurahie tamasha bei ya tiketi kwa kila siku ni shilingi 3,000 kwa watanzania na wageni kutoka nchi za nje ni Dola 48 za kimarekani.
Tamasha la 10 litakutanisha vikundi mbalimbali kama ifuatavyo Cheikh Lô (Senegal) Mlimani Park Orchestra (Tanzania) Khaira Arby (Mali) Comrade Fatso and Chabvondoka (Zimbabwe) Culture Musical Club (Zanzibar / Tanzania) Atongo Zimba (Ghana / UK) N’Faly Kouyaté (Guinea) Nathalie Natiembe (Reunion) Zanzibar Unyago (Zanzibar / Tanzania) Nawal & Les Femmes de la Lune (Comoros / Mayotte) Wazimbo (Mozambique) The Moreira Project (Mozambique / South Africa) Owiny Sigoma Band (Kenya / UK) Mokoomba (Zimbabwe) Msafiri Zawose & Sauti Band (Tanzania) Mani Martin (Rwanda) Burkina Electric (Burkina Faso / USA) Lumumba Theatre Group(Tanzania) Sousou & Maher Cissoko (Senegal / Sweden) Super Maya Baikoko (Tanzania) Peter Msechu (Tanzania) Wakwetu Jazz Vibes (Tanzania) Safi Theatre Group (Tanzania) na wengineo.
Sauti za Busara hufanikiwa kuwaleta wageni wengi kila mwaka, lakini huifadhi misingi ya wenyeji. Hutoa fursa kwa wenyeji kuona na kusikiliza muziki kutoka sehemu mbalimbali za Afrika na vilevile kuutambulisha muziki wa Afrika Mashariki kwa wageni, fursa hii ni adhimu sana kiafya na kimaendeleo ya kimuziki.
Tamasha huwakutanisha watu pamoja kusheherekea na umoja, bila ya kuzingatia itikadi zao za kisiasa na kidini. Fursa kama hii ni adimu sana Zanzibar, na tukio hili limekuwa ni kiungo na muhimu katika kuimarisha umoja na amani, kujenga mahusiano mema na kuheshimiana.
Zaidi ya hayo, siku hizi watu wengi hutafuta mbinu muafaka za kujiwezesha kiuchumi kila, kupitia muziki na sanaa mbalimbali. Kwa matarajio yetu makubwa kabisa kwamba wageni huja kwa wingi na hutegemea kupata vitu adhimu kabisa kutoka kwetu, kama kufurahia muziki wakiwa na wenyeji wao.
Tamasha husaidia ukuwaji wa kiuchumi. Takwimu ya Serikali imeonyesha idadi ya wageni wanaokuja Zanzibar imeongezeka kwa zaidi ya asilimia 500 tangu lilipoanza tamasha.
Tamasha la Sauti za Busara hutoa mfano wa tukio ambalo lenye muundo wa kimaendeleo kwa pande zote wageni na wenyeji, kwa uthamini utajiri wa tamaduni mbalimbali za kiafrika. Huonyesha uzuri wa muziki wa tamaduni za kiafrika, na uwezekano wa kutengeneza ajira na kujiongezea kipato.

Song : Mr.Blue ft Man Walter – Nipende

Wednesday, October 17, 2012

AMTZ to establish online swahli course

Action Music Tanzania (Reg, No.BST 4733) has established Online Swahili lessons for any one who is interested to learn Swahili. The course aims at enabling a leaner to master how to listen, speak, write, and read Swahili language in a short time. There are many ways that we deliver our lesson including skype, you tube and our blog. Any one can choose time for the lesson to take part according to what she/he sees it fit. On the completion of the course you will be awarded with a certificate.
Though people have different reasons for learning Swahili, the most common interests in the language have been: its usefulness for research and travel purposes in East and Central Africa, meeting foreign language requirements in foreign academic institutions; and retracing the roots for the East African people living in Diaspora.
On other hand Swahili has been called a window for accessing East African culture. Many who have studied Swahili as a foreign language are continuously finding it useful in voluntary work and in the job market, especially among the many organizations that are getting involved in several projects in Africa. Many who go ahead to establish organizations working in East and Central Africa, either driven by social entrepreneurial goals or the traditional Aid Organizations, have also attested to its usefulness in penetrating the region.
Welcome and learn Swahili at affordable price. Karibu sana!
For fees structure, booking and scheduling your lesson please contact us by
actionmusictz@gmail.com establish 

Friday, October 12, 2012

DIAMOND: ASANTE SANA MSN KWA HESHIMA HII MLIYONIPA

Honestly nimejiskia furaha sana kuandikwa katika mtandao mkubwa kama huu
juu ya kazi zangu za muziki ninazozifanya, tena kubwa zaidi ni kupewa heshima hii kubwa ya kuwa King of Bongo Flava...kiukweli imenipa matumaini sana ingawa nafsi yangu inaniambia Bado sistaahili kuitwa jina hilo kwani bado nna safari ndefu sana.....

Hakika hii inaonesha ni jinsi gani support yenu mnayonipa kutokana na juhudi ninazozionyesha zinazidi kuzaa matunda  na kufanya muziki wetu wa bongo fleva uzidi kupiga hatua na kufika mbali zaidi......Asante sana Mwenyezi Mungu, Mama na Familia yangu, Management na shukrani kubwa kwako wewe shabiki yangu na mdau mkuu wa muziki huu........Aaaamen!

YVONNE MWALE KUPIGA 'SHOW' KATIKA SHEREHE ZA UHURU WA ZAMBIA

"Confirmed: Yvonne Mwale will perform at the celebrations for Zambia Independance Day, organized by the High Commision of Zambia to Tanzania. Zambians in Dar es Salaam, see you there!"




Monday, July 16, 2012

SERENGETI, MIKUMI, MANYARA TUNASHINDWA NINI KUFANYA HAYA?



Barabara kuu ya Ecoduct De Woeste Hoeve A50, Netherlands; Nchi ya Netherlands inaidadi kubwa ya wanyama zaidi ya 600 ambao hutumia daraja hilo la aina yake kuvuka barabara.



HUU SI UHARIBIFU WA MAZINGIRA?

BREAKING Newzz>>>CHEGE apata ajali mbaya ya gari usiku huu Temeke


BREAKING: Msanii CHEGE apata ajali mbaya ya gari usiku huu Temeke Dar es salaam, ameumia ila gari halifai kabisa. Chanzo ni mtu wa pikipiki
Dj Sek