Friday, November 16, 2012

Busara Promotions yaanda shindano la waandishi wa makala za mtandaoni na magazetini

Wandaaji wa tamasha la kila mwaka la Sauti za Busara, Busara Promotions wameandaa shindano la uandishi wa makala mbalimbali kuhusiana na tamasha hilo zitakazochapishwa mtandaoni na kwenye magazeti na washindi kuzawadiwa zawadi mbalimbali.
Katika taarifa yake kwa waandishi wa habari, Busara Promotions imeandika:
Hii ni stori kwa ajili ya waandishi, wachapishaji na wenye mitandao ya kijamii. Kitu pekee katika tamasha la kumi la Sauti za Busara ambalo litaanza tarehe 14- 17 Februari 2013. Tamasha limefikia muongo mmoja ambalo hakuna mfano wake. Waandishi wanaombwa kutuma makala mitandaoni, blog na wachapishaji wa magazeti.
Mbali na kushapisha na kuweka makala mbalimbali, makala bora na mwandishi/mtunzi bora atazawadiwa fulana ya tamasha, pasi ya bure ya siku zote za tamasha na Posho kama ishara ya shukrani. Tuma kupitia barua pepe hii press@busara.or.tz mwisho tarehe 30/11/2012.
Tunasubiria kupokea makala bora. Tutawapa idhini waandishi bora kuendelea kuweka makala zao, chapisho mbalimbali kwenye blogs na tovuti baada ya tarehe ya mwisho. Makala bora itajadiliwa kutokana na uhalisia, mtazamo na idadi ya mitazamo/maoni kutoka kwa wasomaji na mashabiki.
Kuhusu Sauti za Busara
Sauti za Busara hufanyika kila mwezi wa pili katika kisiwa cha marashi ya karafuu Zanzibar, tamasha hujulikana kama ‘Tamasha rafiki katika sayari ya Dunia’. Katika kuwawezesha wenyeji ili wafurahie tamasha bei ya tiketi kwa kila siku ni shilingi 3,000 kwa watanzania na wageni kutoka nchi za nje ni Dola 48 za kimarekani.
Tamasha la 10 litakutanisha vikundi mbalimbali kama ifuatavyo Cheikh Lô (Senegal) Mlimani Park Orchestra (Tanzania) Khaira Arby (Mali) Comrade Fatso and Chabvondoka (Zimbabwe) Culture Musical Club (Zanzibar / Tanzania) Atongo Zimba (Ghana / UK) N’Faly Kouyaté (Guinea) Nathalie Natiembe (Reunion) Zanzibar Unyago (Zanzibar / Tanzania) Nawal & Les Femmes de la Lune (Comoros / Mayotte) Wazimbo (Mozambique) The Moreira Project (Mozambique / South Africa) Owiny Sigoma Band (Kenya / UK) Mokoomba (Zimbabwe) Msafiri Zawose & Sauti Band (Tanzania) Mani Martin (Rwanda) Burkina Electric (Burkina Faso / USA) Lumumba Theatre Group(Tanzania) Sousou & Maher Cissoko (Senegal / Sweden) Super Maya Baikoko (Tanzania) Peter Msechu (Tanzania) Wakwetu Jazz Vibes (Tanzania) Safi Theatre Group (Tanzania) na wengineo.
Sauti za Busara hufanikiwa kuwaleta wageni wengi kila mwaka, lakini huifadhi misingi ya wenyeji. Hutoa fursa kwa wenyeji kuona na kusikiliza muziki kutoka sehemu mbalimbali za Afrika na vilevile kuutambulisha muziki wa Afrika Mashariki kwa wageni, fursa hii ni adhimu sana kiafya na kimaendeleo ya kimuziki.
Tamasha huwakutanisha watu pamoja kusheherekea na umoja, bila ya kuzingatia itikadi zao za kisiasa na kidini. Fursa kama hii ni adimu sana Zanzibar, na tukio hili limekuwa ni kiungo na muhimu katika kuimarisha umoja na amani, kujenga mahusiano mema na kuheshimiana.
Zaidi ya hayo, siku hizi watu wengi hutafuta mbinu muafaka za kujiwezesha kiuchumi kila, kupitia muziki na sanaa mbalimbali. Kwa matarajio yetu makubwa kabisa kwamba wageni huja kwa wingi na hutegemea kupata vitu adhimu kabisa kutoka kwetu, kama kufurahia muziki wakiwa na wenyeji wao.
Tamasha husaidia ukuwaji wa kiuchumi. Takwimu ya Serikali imeonyesha idadi ya wageni wanaokuja Zanzibar imeongezeka kwa zaidi ya asilimia 500 tangu lilipoanza tamasha.
Tamasha la Sauti za Busara hutoa mfano wa tukio ambalo lenye muundo wa kimaendeleo kwa pande zote wageni na wenyeji, kwa uthamini utajiri wa tamaduni mbalimbali za kiafrika. Huonyesha uzuri wa muziki wa tamaduni za kiafrika, na uwezekano wa kutengeneza ajira na kujiongezea kipato.

Song : Mr.Blue ft Man Walter – Nipende

Wednesday, October 17, 2012

AMTZ to establish online swahli course

Action Music Tanzania (Reg, No.BST 4733) has established Online Swahili lessons for any one who is interested to learn Swahili. The course aims at enabling a leaner to master how to listen, speak, write, and read Swahili language in a short time. There are many ways that we deliver our lesson including skype, you tube and our blog. Any one can choose time for the lesson to take part according to what she/he sees it fit. On the completion of the course you will be awarded with a certificate.
Though people have different reasons for learning Swahili, the most common interests in the language have been: its usefulness for research and travel purposes in East and Central Africa, meeting foreign language requirements in foreign academic institutions; and retracing the roots for the East African people living in Diaspora.
On other hand Swahili has been called a window for accessing East African culture. Many who have studied Swahili as a foreign language are continuously finding it useful in voluntary work and in the job market, especially among the many organizations that are getting involved in several projects in Africa. Many who go ahead to establish organizations working in East and Central Africa, either driven by social entrepreneurial goals or the traditional Aid Organizations, have also attested to its usefulness in penetrating the region.
Welcome and learn Swahili at affordable price. Karibu sana!
For fees structure, booking and scheduling your lesson please contact us by
actionmusictz@gmail.com establish 

Friday, October 12, 2012

DIAMOND: ASANTE SANA MSN KWA HESHIMA HII MLIYONIPA

Honestly nimejiskia furaha sana kuandikwa katika mtandao mkubwa kama huu
juu ya kazi zangu za muziki ninazozifanya, tena kubwa zaidi ni kupewa heshima hii kubwa ya kuwa King of Bongo Flava...kiukweli imenipa matumaini sana ingawa nafsi yangu inaniambia Bado sistaahili kuitwa jina hilo kwani bado nna safari ndefu sana.....

Hakika hii inaonesha ni jinsi gani support yenu mnayonipa kutokana na juhudi ninazozionyesha zinazidi kuzaa matunda  na kufanya muziki wetu wa bongo fleva uzidi kupiga hatua na kufika mbali zaidi......Asante sana Mwenyezi Mungu, Mama na Familia yangu, Management na shukrani kubwa kwako wewe shabiki yangu na mdau mkuu wa muziki huu........Aaaamen!

YVONNE MWALE KUPIGA 'SHOW' KATIKA SHEREHE ZA UHURU WA ZAMBIA

"Confirmed: Yvonne Mwale will perform at the celebrations for Zambia Independance Day, organized by the High Commision of Zambia to Tanzania. Zambians in Dar es Salaam, see you there!"




Monday, July 16, 2012

SERENGETI, MIKUMI, MANYARA TUNASHINDWA NINI KUFANYA HAYA?



Barabara kuu ya Ecoduct De Woeste Hoeve A50, Netherlands; Nchi ya Netherlands inaidadi kubwa ya wanyama zaidi ya 600 ambao hutumia daraja hilo la aina yake kuvuka barabara.



HUU SI UHARIBIFU WA MAZINGIRA?

BREAKING Newzz>>>CHEGE apata ajali mbaya ya gari usiku huu Temeke


BREAKING: Msanii CHEGE apata ajali mbaya ya gari usiku huu Temeke Dar es salaam, ameumia ila gari halifai kabisa. Chanzo ni mtu wa pikipiki
Dj Sek

Saturday, July 14, 2012

Afande Sele azijibu shutuma za 20 Percent


Uswahiba kati ya wasanii wawili wa Bongo Flava nchini, Afande Sele na 20 Percent umeingia dosari baada ya kutupiana maneno kila mmoja kwa nyakati tofauti kwenye vyombo vya habari.

Maneno hayo yalianza wiki iliyopita baada ya Afande Sele kuzungumza na Clouds FM na kudai kusikitishwa na kitendo cha swahiba wake 20 Percent cha kugoma kutumbuiza kwenye tuzo za muziki za Zanzibar wakati alikuwa amelipwa pesa zote.

Kufuatia mgomo huo, waandaaji walimpeleka lock-up msanii huyo na kubaki na laptop yake mpaka pale atakapowarudishia waandaji hao shilingi milioni moja waliyompa kwaajili ya kuperform kwenye tuzo hizo.

Hatimaye jana 20 Percent alizungumza na kituo hicho cha radio kuhusiana na tukio lenyewe na kusema kuwa Afande Sele amechanganyikiwa na anasumbuliwa na njaa ndio maana anamlaumu.

Akiongea kwa jaziba, 20 Percent amesema Afande Sele ni kama ‘mtoto’ na alimshangaa kufahamu kuwa alifika Zanzibar saa sita usiku bila kuwa sehemu ya kulala kutokana na waandaaji hao kuwa wababaishaji.

Leo (July 14) Afande Sele ametoa maelezo marefu kuhusiana na sakata hilo kupitia Facebook. Hivi ndivyo alivyoandika:

“Salaam Ndugu zangu wote mashabiki na wadau wa muziki wetu!!
Tamko langu kuhusiana na lugha zilizotolewa na Twenty Percent kuhusiana na show yetu ya Zanzibar Music Award.

Tulialikwa kwenye ZANZIBAR MUSIC AWARD, na kabla ya kazi makubaliano yote ya kazi kwa mujibu wa mkataba yalifuatwa, makubaliano hayo yalihusisha sisi kujigharamia gharama zote za nauli na Malazi (accomodation).

Tulifika Zanzibar salama, tulipokua Zanzibar twenty alitaka agharamiwe huduma zote ambazo ni nje ya mkataba wetu, nikamuomba na kumsihi sana ndugu yangu aheshimu mkataba, asitafute matatizo kwani tayari mpaka wakati huu tuna kesi na Halmashauri ya Manispaa ya Moro ambayo kimsingi sikuhusika (nilishatolea ufafanuzi siku za nyuma).

Lakini yeye alipingana na mimi, akanibishia na kunisukuma Mbele ya wageni na wenyeji wetu, wakiwemo Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seiph Ali Idi, Waziri Seiph Khatibu.

Walikuwepo waadishi wa habari wa siku Nyingi Akiwemo Abubakari Liongo (idhaa ya kiswahili radio Ujerumani), Mkurugenzi wa ZENJI FM ndugu Tua Saidi Tua.
Mimi Selemani Abdallah Juma Msindi sihusiki kwa namna yoyote, na tabia zisizo za kuridhisha zinazoonyeshwa na Ndugu yangu Twenty Percent, ambae nimekua nae nyumbani kwangu hata kabla ya Tuzo zake Tano (Kili Music Award) ambazo kazi hizo zote hizo kaandikia nyumbani kwangu siwezi kuwa na tatizo nae ni ndugu yangu kiimani na kikazi, hata kazi yangu niliyofanya nae kabla siku za nyuma "MBELE YAKO NYUMA YANGU" .. Kuna mstari Nilisema " ..Kuandika Rhyme kwenda Gym kimtindo kuonyesha Ugumu, bado unatakiwa uwe na nidhamu ya kweli, sio ya kumzuga Mwalimu, utajihukumu".

Nimekua nikisisitiza nidhamu kwa Ndugu zangu woote toka enzi za Ghetto BoyZ, Watupori na Mabwasha'Kingdom, ambao wengine hawafanyi sanaa, ila nipo nao kwenye Familia yetu kubwa hapa Tanzania. Nimesikitishwa na kitendo hicho. Siku zote nimekua mwenye kuhitaji suluhu kwa namna ya Amani.

Verry sorry kwa wote ambao mmefadhaika kwa hilo. Tuendelee kuwa pamoja na msisite kutoa ushauri wenu, maoni ili Game letu lisonge. MUNGU ATUBARIKI.
Asanteni sana.

Selemani Juma Abdallah Mutabhazi Msindi.
a.k.a Afande Sele (King of Rhymes)

Chanzo: Leotainment blog

MAFANIKIO YA CHAMELEONE KATIKA MAISHA


.
Baada ya kukutana na staa wa muziki kutoka Uganda Jose Chameleone nimegundua kuna mambo mengi nilikua nayasikia tofauti na kuyasoma ambayo yeye ameyazungumza tofauti kabisa.
Nilikua sijui, kumbe Chameleone alianza kuenjoy kuwa staa kuanzia mwaka 2000 japo alianza muziki 1995, 2003/2004 ndio alianza kupata pesa na hapo ndipo maajabu yalianza kutokea kwa kuanza kutimiza ndoto.



Jose Chameleone hapa akiwa  na Millard Ayo wa  Clouds
Chameleone amesema “nilijenga nyumba yangu kwa miaka miwili ambapo 2005 ilimalizika na ikawa imegharimu shilingi milioni 200 -300 za kitanzania, wakati nilikua naijenga hiyo ndio pesa niliyokua nayo na nikasema kabla sijaipoteza acha nifanye kitu muhimu lakini Mungu akanibariki tena baada ya kujenga hiyo nyumba nikapata bahati nyingine nikaendelea na vitu vingine”

Jose Chameleone (katikati) akiwa kwenye shooting ya moja ya video 

Exclusive na millardayo.com Mwimbaji huyu staa kutoka Uganda amesema vyanzo vyake vikubwa vya mapato kwa sasa ni kununua na kuuza ardhi, kuuza simu za mkononi ziitwazo Chameleone anazozitengeza China, kununua nyumba na kuziuza pia kupangisha nyumba.
kuhusu vyanzo vingine vya mapato Chameleone amesema “show pia zinatulipa sana Uganda japo siwezi kukwambia nalipwa bei gani kwa sababu sipendi kuonekana mtu wa kujisifia lakini kwa wiki moja naweza kupiga show mbili Kampala au Uganda, na kingine kinachotulipa sana ni Kampuni kubwa za biashara ambazo zikikuona una nguvu zinakuchukua na kukulipa vizuri kwa kufanya nao promoshen au mambo mengine ya mkataba wa biashara”



Hii ni kwa  Hissani ya  www.millardayo.com

Friday, July 13, 2012

MAFUNZO YA MUZIKI 2012


Tuesday, July 3, 2012

MAFUNZO YA KUPIGA ALA ZA MUZIKI

ACTION MUSIC TANZANIA (AMTZ) YENYE NAMBA YA USAJILI BST/4733 ITATOA MAFUNZO YA UPIGAJI WA ALA MBALIMBALI ZA MUZIKI (KWA VITENDO) KWA WATU WOTE

MAFUNZO YATAANZA: TAREHE 16/07/2012

MAHALI: IDARA YA SANAA NA SANAA ZA MAONESHO (FPA) CHUO
                     KIKUU CHA DAR ES SALAAM (SEHEMU YA MLIMANI)

NJOO UJIFUNZE MBINU ZA KITAALAMU ZA KUPIGA/KUCHEZA  GITAA, KEYBOARD/PIANO, TARUMBETA, SAXOPHONE, KONGA, DRUM SET, NA UPIGAJI WA NGOMA ZA ASILI YA TANZANIA, BILA KUSAHAU MAFUNZO MAALUMU YA “BODY PERCUSSION” (Matumizi ya mwili kutengeneza midundo ya muziki) NA USOMAJI WA “NOTATION” YATAKAOTOLEWA NA WATAALAM WALIOBOBEA KATIKA TASNIA YA MUZIKI KUTOKA VYUO MBALIMBALI.

USAJILI UNAFANYIKA: IDARA YA SANAA NA SANAA ZA MAONESHO (FPA) CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (MLIMANI)
FOMU ZA USAJILI ZINAPATIKANA FPA SAA 4:00 ASUBUHI HADI SAA 10:00 JIONI KWA GHARAMA YA SHILINGI 3000/= TU. WAHI, NAFASI NI CHACHE.

KWA MAWASILIANO:  +255 757 361 266
                                                +255 714 553 239
                                                +255 755 058 045
E-mail: actionmusictz@yahoo.com/mandolintz@yahoo.co.uk/mpepodamas@gmail.com
www.actionmusictz.blogspot.com

NYOTE MNAKARIBISHWA

Saturday, June 30, 2012

Exclusive uchambuzi: Wazazi wa Dogo Janja fuatilieni maendeleo yake, msiwaachie Mapromota

Dogo Janja
Na Dotto Kahindi-Thisday Magazine, Blog za mikoa

Mwezi Juni mwaka huu umekuwa ni mwezi wa huzuni na furaha kwa nyota wa muziki wa Bongo Fleva , Abdul Abubakar Chande ‘Dogo Janja’ kufuatia kutimuliwa na Baba yake kimziki Madee na baada ya siku chache kurejea Dar es Salaam na kuingia mkataba mpya na kampuni ya Mtanashati Entertainments.
Dogo Janja alitimuliwa na Madee na kurejeshwa kwao jijini Arusha kwa madai ya kushindwa kuzingatia masomo kwa kuendekeza utoro shuleni, kukosa mwenendo mwema kimaadili sababu ambazo hata hivyo Dogo Janja alizikanusha na kudai kuwa alikuwa akinyanyaswa na Madee.
Alidai kuwa akiwa chini ya usimamizi wa Madee alikuwa akilipwa posho kidogo baada ya kufanya maonyesho na kwamba Madee alihusika kumwibia pesa zake benki hali iliyomfanya kuwa na salio la Tsh.25, 000 elfu tu katika akaunti yake.
Hali ilikuwa hivyo na imeleta picha mbaya na kuibua maswali mengi kwa mashabiki wa muziki lakini lawama kubwa zinafaa kupelekwa kwa wazazi wa Dogo Janja ambao walimruhusu kwa moyo mweupe aje kuishi na watu ambao leo hii wanaonekana kuwa ni wahuni.
Pamoja na kutimuliwa na Madee lakini sasa sasa amerejea tena akiwa katika mwonekano mwingine, naamini muda mfupi aliokaa na wazazi wake walifanya mazungumzo ya kutosha na kufanya makubaliano ya nini kipewe kipaumbela katika maisha yake kwa sasa, ili kumjengea mafanikio yake kielimu na kimaisha pia.
Furaha aliyoipata baada ya kutua Bongo na kujiunga na kampuni ya Mtanashati Entertainments ya jijini Dar es Salaam, zisimfanye akajisahau tena na kuendeleza upuuzi alioufanya akiwa na Madee.
Tukubaliane wote kuwa Dogo Janja bado ni mtoto na anahitaji kupata mwongozo wa kutosha kutoka hasa kwa wazazi wake na watu walio juu ya uwezo wake ili kumsaidia kufanya kila hatua kwa usahihi asije kujuta baadaye.
Pengine kwa hatua ya nyota huyo cha kwenda kusomewa kisomo maalumu cha kuomba Mwenyezi Mungu amnyooshee mambo yake pindi atakapoanza kushusha ngoma mpya kinaweza kuonyesha kuwa kuna nia njema kwa watu alionao sasa.
Maneno ya Mkurugenzi wa kampuni hiyo Ostaz Juma na Musoma kuwa wameamua kumfanyia kisomo hicho kwa lengo la kuweka kazi zote za Dogo janja mikononi mwa Mungu ili kumkinga na watu wabaya ambao kwa namna moja ama nyingine hawajafurahishwa na mpango mzima wa dogo huyo kurejea Bongo.
Hata hivyo katika kipindi kifupi alichojiunga na kampuni hiyo Dogo janja amefanyiwa ‘shopingi’ ya nguvu kwenye maduka makubwa ya viwalo yaliyopo Mlimani City jijini Dar ambayo ilitumia zaidi ya shilingi Milioni 2.5.
Hivi ni miongoni mwa vitu vinavyomfanya Dogo Janja afurahie kuwa katika kampuni hiyo lakini lazima ajue kuwa nidhamu ya kazi ndiyo itamfanya aendelee kupata matunda hayo maana akiendelea kujifanya nunda na kupuuza ya wakubwa wake haitamsaidia.

Monday, February 27, 2012

2012 with new talents



Friday, December 23, 2011

TANGAZO! TANGAZO! TANGAZO!

ASASI YA ACTION MUSIC TANZANIA (AMTZ) YENYE NAMBA YA USAJILI BST/4733 IMEANDAA NA ITAENDESHA MAFUNZO YA MUZIKI (NADHARIA NA VITENDO) KWA WATU WOTE KUANZIA TAREHE 09/01/2012 IDARA YA SANAA NA SANAA ZA MAONESHO (FPA) CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.

USAJILI UNAFANYIKA KATIKA OFISI ZETU (AMTZ) ZILIZOPO SHULE YA MSINGI MWENGE KARIBU NA MARYLAND BAR, KILA SIKU KUANZIA 20/12/2011 HADI 7/1/2012, SAA 4:00 HADI SAA 7:00 MCHANA, NA SAA 8:00 HADI SAA 11:00 JIONI. FOMU ZA USAJILI ZINAPATIKANA OFISINI KWA GHARAMA YA SHILINGI 3000/= TU

MAFUNZO YATAKAYOTOLEWA NI PAMOJA NA NADHARIA YA MUZIKI, UCHEZAJI/UPIGAJI WA ALA ZA MUZIKI ZIKIWEMO GITAA, KEYBOARD/PIANO, TARUMBETA, SAXOPHONE, KONGA, DRUM SET, NA UPIGAJI WA NGOMA ZA ASILI YA TANZANIA.

PIA YATATOLEWA MAFUNZO YA “BODY PERCUSSION” (Matumizi ya mwili kutengeneza midundo ya muziki)

KWA MAWASILIANO:-
                        +255 757 361 266
                        +255 716 515 853
                        +255 755 058 045
E-MAIL: actionmusictz@yahoo.com
www.actionmusictz.blogspot.com
 


Wednesday, September 21, 2011

MAFUNZO YA MUZIKI AGOSTI 2011, FPA, UDSM

Mwalimu wa muziki wa AMTZ Abeid Mussa akitoa maelekezo wakati mafunzo upande wa 'Music Ensemble'

Washiriki wa mafunzo ya muziki yaliyofanyika Agosti 8-21, 2011 wakifanya onyesho, katika kituo cha utamaduni cha Ujerumani, Goethe Institut-Tanzania kilichopo Upanga, Dar es Salaam