Wednesday, July 2, 2014

Professor J aongea na COSOTA kuhusu utaratibu wa Radio na TV kuwalipa wasanii kwa kucheza kazi zao

Msanii wa Hip Hop, Joseph Haule aka Professor J jana amekitembelea chama cha haki miliki Tanzania, ‘COSOTA’ na kuwauliza kwanini Radio na TV za Tanzania haziwalipi wasanii pindi wanapoziga nyimbo zao kwenye vituo vyao.
Professor-Jay1-copy-800x596
Professor ameiambia Bongo5 kuwa baada ya kupeleka shauri hilo, wahusika ambao ni COSOTA wamesema bado wapo kwenye vikao kujadili suala hilo.

“COSOTA sio watu wa mwisho, wameniambia kuna vikao vingine vinaendelea, tuweke subira lakini hili suala linajadiliwa kila siku. Budget ya serikali imepita hakuna kilichoendelea, kama ni matatizo yapo kwenye sheria kwanini isirekebishwe? Lakini tuseme kweli haya mambo yanatakiwa yaanze ingawa kumekuwa na changamoto. Hata wasanii wenyewe wanafanya muziki kama muziki ilimradi wanajifurahisha, lakini kama watakuwa serious vyombo vya habari ‘Radio na TV’ kwa kuwalipa wasanii, maana yake hata wasanii wenyewe watakuwa serious kufanya muziki kwa perfect na itachuja upi mchele zipi pumba, naamini hivyo,” amesema.


“Vyombo vya habari haviwezi kukubali kumlipa mtu ambaye yupo shaghalabaghala ambao hawafanyi muziki ambao unaeleweka. Kenya wenzetu wanalipwa, nimekuawa nikishauriana na wasanii wa Kenya kuhusu hili suala, wakaniambia Kenya kuna baadhi ya wasanii ambao wapo kwenye COSOTA yao, kwahiyo inakuwa ni rahisi wenyewe kuangalia ni jinsi gani wasanii wao wananufaika na muziki wao. Kwetu hapa hili swala likipita kwanza wasanii watanufaika na kazi zao pamoja na serikali itanufaika, pia Radio na TV wakitaka wanufaike na muziki wa wasanii watadili na matangazo, sio kama sasa hivi, TV na Radio zinaingiza pesa nyingi kwa matangazo kutokana na kupiga nyimbo zao kwenye vipindi vyao,” aliongeza.

Professor amewataka wasanii wengine kuungana katika kulifuatilia suala hilo.
“Kinachoonekana kwa wasanii wengi wa Bongo tunaogopa kumfunga Paka kengele, wengi tunaogopa wakati muziki ndo wenye manufaa kwetu. Sasa hivi na baadaye, wazee wetu akina mzee Marijani, Remmy Ongara mwenyezi Mungu amlaze mahali pema, wao tayari wakati wao umepita, sasa hivi ni jukumu letu kuutoa muziki hapa ulipo na kuupeleka kwenye next level na kuwafanya watu wote waweze kunufaika kwa njia moja ama nyingine, ukiangalia kwenye TV wana matangazo kibao hayo yote yapo kwa manufaa yao kwanini na mwanamuziki asinufaike.”

Tuesday, April 29, 2014

FURSA: MAFUNZO YA KUPIGA ALA ZA MUZIKI KUANZA TENA MWEZI MEI

 Baadhi ya wanafunzi wakiwa kwenye mazoezi

Action Music Tanzania (AMTz) inatangaza fursa kwa watu wote kujiunga na mafunzo ya kupiga ala za muziki yanayoanza tarehe 3/5/2014, lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wanamuziki wa kupiga ala na kufanya maonesho kwa weledi na utaalamu zaidi.
Baadhi ya wanafunzi wakiwa darasani

Mafunzo yanayotolewa ni pamoja na upigaji wa ala za muziki zikiwemo gita, kinanda, tarumbeta, saxophone, konga, drum set, na upigaji wa ngoma za asili. Pia yatatolewa mafunzo ya ‘body percussion’ yaani matumizi ya mwili katika kutengeneza midundo ya muziki.

Mafunzo hayo yanafanyika kwenye ofisi za AMTZ zilizopo maeneo ya Mwenge mtaa wa Umoja, nyuma ya magorofa ya jeshi na kwenye Idara ya Sanaa na Sanaa za Maonesho Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo ili kujiunga na mafunzo haya wasiliana nao kwa simu namba 0686928828/0653075791 ili kupata fomu za kujiunga na mafunzo.

Monday, March 3, 2014

ONESHO LA WAPIGA ALA/VYOMBO VYA MUZIKI KUFANYIKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM SIKU YA IJUMAA

Action Music Tanzania inayofuraha ya kukualika kuhudhuria onesho la muziki litakalofanyika siku ya Ijumaa ya tarehe saba mwezi wa tatu (07.03.2014) kwenye idara ya sanaa na sanaa za maonesho (FPA) Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzia saa kumi na mbili na nusu jioni hadi saa mbili usiku (12:30-2:00), Kiingilio ni bure.
Onesho hilo limeandaliwa na AMTZ litawahusisha wanamuziki kutoka kwenye taasisi mbalimbali ambao wameshiriki mafunzo maalumu ya muziki kwa muda wa wiki mbili ambayo yamefanyika kwenye Idara ya Sanaa na Sanaa za Maonesho ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (FPA), kuanzia Februari 24 mwaka huu. Pia wakati wa onesho kutakuwa na zoezi la kuchangia mfuko wa AMTZ ambapo wageni wataombwa kuchangia kiasi chochote cha fedha ili kuijengea uwezo asasi wa kuendelea kutoa mafunzo ya namna hiyo kwa watu wengine.
AMTZ ni asasi isiyo ya kiserikali inayoundwa na walimu wa muziki kutoka katika taasisi mbalimbali za elimu ya muziki nchini na imesajiliwa na BASATA na kupata kibali cha kutoa mafunzo ya muziki ya muda mfupi. AMTZ imekuwa ikitoa mafunzo ya muziki kwa wanamuziki wa aina zote kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kuandaa, kucheza na kufundisha muziki kwa kutumia mbinu mpya na za kitaalamu ili kuambukiza elimu ya muziki kwa wanamuziki wengine na hatimaye kuboresha ustawi wa muziki kwa ujumla wake nchini.
Kufika kwako katika onesho hilo utakuwa ni mchango mkubwa sana kwa wanamuziki wetu, asasi yetu na muziki kwa ujumla wake. Natanguliza shukran zangu za dhati na karibu sana

Contact:
Mandolin Kahindi
Executive Secretary
Action Music Tanzania

Monday, December 16, 2013

FURSA: MAFUNZO YA KUPIGA ALA ZA MUZIKI

Action Music Tanzania (AMTZ) inatangaza fursa kwa watu wote kujiunga na mafunzo ya kupiga ala za muziki yanayoanza desemba 19 mwaka huu, lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wanamuziki wa kupiga ala na kufanya maonesho kwa weledi na utaalamu zaidi.

Mafunzo yanayotolewa ni pamoja na upigaji wa ala za muziki zikiwemo gita, kinanda, tarumbeta, saxophone, konga, drum set, na upigaji wa ngoma za asili. Pia yatatolewa mafunzo ya ‘body percussion’ yaani matumizi ya mwili katika kutengeneza midundo ya muziki.

Mafunzo hayo yanafanyika kwenye ofisi za AMTZ zilizopo maeneo ya Mwenge karibu na magorofa ya jeshi ambapo ili kujiunga na mafunzo haya wasiliana nao kwa simu namba 0686928828 au barua pepe, actionmusictz@yahoo.com, Like Facebook Page au tembelea www.amtz.org
 Mwalimu Abeid Mussa akitoa maelekezo ya wakati wa mazoezi ya kufanya onyesho la muziki
 Mwalimu wa Kinanda Prosper Shirima (katikati) akifundisha
Mwalimu wa Gita, Ashimba (kushoto) akitoa maelekezo ya namna ya kupiga chombo hicho

Thursday, December 12, 2013

Arts and culture contribute more to U.S. economy than tourism

For the first time the federal government has tallied up the arts and culture contribution to the nation’s economy. It turns out that sector, movies, painting, publishing, cable and more, was worth half a trillion dollars -- 3 percent to the gross domestic product in 2011. That’s more than the travel and tourism industry.
“Here you have for the first time, comprehensive empirical evidence from the point of view of economists that the arts play a substantial role in the nation’s economy,” says Sunil Iyengar who runs the Office of Research and Analysis for the National Endowment for the Arts.
In an instant, writers, app designers, publishers and painters just got a bunch of "street cred." Nearly two million people work in the arts and culture industry which exported about $40 billion in goods and services in 2011. Some economists say ideas, innovation, and creativity are essential to growing the United States economy.
University of Minnesota culture economist Ann Markusen says putting a dollar value to the sector could lead to policies that promote it. “The recognition of the significance of art skills, is going to really be a big boost for artists and also for encouraging young people to go into the arts,” she says.
Who knows, maybe that whole starving artist thing will finally be on its way out.

Tuesday, December 10, 2013

TANGAZO: WANATAFUTWA WAIMBAJI CHIPUKIZU WA MUZIKI WA UNJILI

HABARI   NJEMA   KWA   WAIMBAJI  CHIPUKIZI  WA  MUZIKI   WA    INJILI  TANZANIA.

Wewe ni  kijana  wa  kikristo  uliye  okoka ?
Una  karama  ya  uimbaji ?
Unataka  kumtumikia  na  kumtangaza  Mungu  kwa  njia  ya  uimbaji  ?
Kama  jibu  ni  ndio  basi  hii  ni  habari  njema  sana  kwako.
Huduma  Ya  UPENDO  & FURAHA  ya  jijini  Dar  Es  salaam, inatafuta  vijana  wa  kikristo    walio  okoka, kwa  ajili   ya  kuanzisha  huduma ya  muziki  wa  injili  itakayo  kuwa  ikihudumu  katika  mikoa mbalimbali  ya Tanzania  na  katika  nchi  jirani.
SIFA   ZA   WATU   WANAO   HITAJIKA  :
i.             Awe  na  karama  ya  uimbaji
ii.            Awe  na  Umri   wa   kuanzia  miaka  16  hadi  35.
iii.          Awe  ameokoka  na  mwenye  hofu  kuu  ya  Mungu.
iv.           Awe  na  wito  wa  kweli   wa  kumtangaza  na  kumtumikia  Mungu  kwa  njia  ya  uimbaji.
v.             Awe  na  utayari , pamoja  na   muda  wa  kutosha   wa  kusafiri  na  huduma  katika  mikoa mbalimbali  ya  Tanzania  pamoja  na  nchi  jirani.
vi.           Awe  mkazi  wa  Dar  Es  salaam .

USAILI  utafanyika  siku  ya  tarehe  06  January  2013.
MWISHO  wa  kujiandikisha  ni  tarehe  24  Desemba  2013.
Kujiandikisha,  fika  moja  kwa  moja  ofisini  kwetu, siku za  kazi kuanzia  saa  tatu kamili  asubuhi  hadi  saa kumi  kamili  jioni, au   wasiliana  nasi  kwa   SIMU   0784406508

Thursday, June 27, 2013

British Council yatoa mafunzo ya uongozi na biashara kwa viongozi wa taasisi za sanaa na sanaa za maonesho

 Washiriki katika mafunzo ya uongozi na biashara yananofanyika kwenye Ukumbi wa Nafasi Jijini Dar es Salaam wakifuatilia mafunzo hayo, washiriki hao wametoka katika taasisi mbalimbali zinazojishughulisha na sanaa na sanaa za maonesho.



Mafunzo haya yanatolewa na Britishi Council, na mwezeshaji ni Faisal Kiwewa kutoka shirika la Bayimba la nchini Uganda.

Tuesday, May 14, 2013

GOETHE INSTITUT-TANZANIA INVITE YOU TO AN OPEN STAGE NIGHT




On our OPEN STAGE NIGHT we invite you to perform. Whatever your talents might be, everyone is welcome to show them on stage. Please register now by sending us an e-mail or call us.E-mail: intern@daressalaam.goethe.org, Tel.:  075 375 152 and Tell us what you are planning to perform and the required technical equipment. 

Musicians can also bring their own instruments. entrance is fees.




Monday, May 13, 2013

USAJILI WA TUZO ZA MUZIKI ZA RFI WAANZA, WANAMUZIKI TANZANIA CHANGAMKIENI FURSA HII


Kwa usajili wa tuzo za muziki za rfi ambazo hufanyika kila mwaka na kuwashirikisha wanamuziki mbalimbali katika bara la Afrika bonyeza hapo chini rfi music award registration

Friday, May 10, 2013

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA SEMINA YA SOKO LA MUZIKI AFRIKA MASHARIKI 'DOADOA' JINJA UGANDA


 Washiriki katika semina ya kujadili changamoto za soko la muziki Afrika Mashariki wakifuatilia moja ya mada kwenye hotel ya Crasted Crane mjini Jinja, Uganda
 Mwanmuziki kutoka Kenya, Winyo akitumbuiza katika moja ya matamasha yanayoambatana na semina ya kujadili changamoto katika soko la muziki Afrika Mashariki.
 Wanamuziki wakiimba wimbo wa ushirikiano katika moja ya matamasha yanayoambatana na semina ya kujadili changamoto katika soko la muziki Afrika Mashariki, kutoka kushoto ni Mani Martin kutoka Rwanda, Shamsila kutoka Arusha Tanzania na Staffi kutoka Uingereza.


Kwa picha za matukio zaidi tembelea DOADOA 2013

Wednesday, May 8, 2013

SEMINA YA KUJADILI CHANGAMOTO ZA SOKO LA MUZIKI AFRIKA MASHARIKI 'DOADOA' YAFANYIKA UGANDA

Waendesha mada katika semina ya kuangalia changamoto katika soko la muziki Afrika Mashariki na njia za kuzitatua wakijadili umuhimu wa elimu ya muziki katika soko la muziki, kutoka kulia ni Katibu Mtendaji wa Action Music Tanzania, Mandoli Kahindi, Mkurugenzi wa sanaa kutoka Global Music Academy Ujerumani,William Ramsay, Muaandaaji wa muziki wa Uganda, Kazi Kasozi na Mkurugenzi Mtendaji wa Ketebul Music Kenya, Tabu Osusa


Semina hiyo ambayo inaambatana na maonyesho ya kazi mbalimbali za muziki yameandaliwa na Bayimba Cultural Foundation ya Uganda ambapo wadau mbalimbali wa muziki kutoka nchi mbalimbali wamejumuika kujadili na kubadilishana uzeofu juu ya soko la muziki kwa nchi za Afrika Mashariki. picha za matukio zaidi tembelea DOADOA

Wednesday, November 21, 2012

Exclusive Photos: Behind the scenes ya video mpya ya Makamua – Bado Kujuana

makamu (600x338)
makamua1 (600x338)
makamua3 (600x338)
makamua4 (600x338)
makamua5 (600x338)
makamua7 (600x338)
Love scene ilianzia hapa
Dr Eddo akitazama kitu
MMhhh
hapa nisaidie wewe
Dr Edooo
how deep is your love for me
Makamua akiwa amezungukwa na warembo

Makamua ametoa picha exclusive za behind the scenes ya video yake mpya inayotarajiwa kutoka rasmi leo. Picha hizi ni za wimbo wake mpya “Bado Kujuana” ambayo amemshirikisha msanii mwenzake Dr Eddo ambaye ndiye aliyefanya production zote mbili za audio na video ambapo picha zote za video zimechukuliwa jijini Mwanza.

Video : King Zilla ft Marco Chall – Nataka


SKYLIGHT BAND YAZIDI KUCHENGUA MASHABIKI @ THAI VILLAGE - MASAKI JIJINI DAR.

Pichani Juu na Chini Mashabiki wa SKYLIGHT BAND wakisakata mduara kwa raha zao katika ukumbi wa Thai Village jijini Dar es salaam.

Sunday, November 18, 2012

JB Mpiana kufanya Onyesho Dar Novemba 30

Mkurugenzi wa QS Muhonda J Entertainment, Joseph Muhonda (katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) katika ukumbi wa Millennium Business Park, Kijitonyama jijini Dar es Salaam mapema leo asubuhi wakati akizungumzia onyesho la Mwanamuziki wa Kimataifa kutoka nchini Congo,JB Mpiana kwa kushirikiana na Mashujaa Band litakalofanyika katika viwanja vya Leaders Novemba 30. Wengine kulia ni rais wa Mashujaa, Chaz Baba na kushoto ni Mshauri wa bendi, King Dodo.

Rose Muhando Kutikisa Tamasha la Shangwe Kagera

MWIMBAJI maarufu wa muziki  wa Injili nchini, Rose Muhando na mwenzake Enock Jonas (Zunguka) wanatarajiwa kutia chachandu katika tamasha la kwanza kubwa kufanyika Mkoani Kagera.
Tamasha hilo la Shangwe Kagera lina lengo la kuielimisha jamii na kuamsha mwamko wa kusaidia watoto yatima na wanaoishi katika maisha magumu.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Beula Communications Ltd, ambao ni waandaji wa tamasha hilo,Melkizedeck Mutta anasema kuwa matayarisho ya tamasha hilo yanaendelea vizuri kutokana na mwitikio mkubwa wa watu mbalimbali waliojitokeza kushiriki.
Pia, Mutta anasema bendi ya muziki ya wazawa mkoa huo, Kakau Band pamoja na vikundi vingine vya wanakwaya  wa makanisa mbalimbali, kikundi cha watoto yatima wanatarajia pia kutumbuiza.
Mutta anasema tamasha hilo la aina yake  linatajiwa kufanyika  Uwanja wa Kaitaba na pia kwenye ukumbi wa Lina’s mjini Bukoba, siku ya Uhuru, Desemba 9.
“Mpaka sasa tumekamilisha sehemu kubwa ya matayarisho hayo ikiwamo kulipia  uwanja pamoja sehemu ya malipo kwa wasanii ambao watashiriki,” alisema.
Pia, mkurugenzi huyo aliwaomba wadhamini zaidi na wadau wengine wa maendeleo na watoto kujitokeza kushiriki ili kuwasaidia jamii hasa watoto yatima na wengine wanaoishi katika mazingira magumu.
 Ni kuhamasisha jamii kuishi kwa amani,kupendana na kusaidia watu wengine hasa wasiojiweza kimaisha  ili na wao wajione ni sehemu yao.
Katika  kutambua hilo kampuni yetu iliamua kufanya utafiti mdogo nakugundua changamoto nyingi katika Mkoa wa Kagera, mojawapo ni kuwa na  watoto wengi wanaoishi katika mazingira magumu. Baada ya kuliona hili, tulitembelea vituo mbalimbali vya kulelea watoto hao, mojawapo ni Tumaini Children’s Centre   kinachomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Ki lutheri Tanzania (KKKT).
Kituo hiki kinalea watoto wote bila kujali kabila,jinsia wala dini zao,  kwa sasa kituo hiki kinahudumia watoto zaidi ya 800, kwa kuwapatia elimu,chakula, malazi n.k  ambapo kwa muda mrefu kimekuwa kikipata msaada toka Sweden ambao kwa sasa wametangaza kuusitisha kwa maelezo kuwa jamii ya Watanzania inapaswa kujifunza na kuanza kuhudumia watu wao wenyewe.
Kutokana na hilo ndiyo maana tumeonelea tuwe na tamasha la kuamasisha jamii ili ianze kuona umuhimu wa kusaidia  wenzao wanaohitaji msaada.

Saturday, November 17, 2012

Alliance Francois na onesho la utamaduni

na Khadija Kalili.
KITUO cha Utamaduni cha Ufaransa ‘Alliance Francois’ kimeandaa onesho la bure la muziki wa utamaduni wa Mwafrika katika kituo chake kilichoko Barabara ya Ali Hassan Mwinyi, jijini Dar es Salaam leo jioni.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa kituo hicho, Michael Shuma, aliwataja wasanii watakaonogesha onesho la leo kuwa ni Maryse Ngalula kutoka Kinshansa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Elie Kamano ‘General Kamano’ wa Guinea, ambaye anapiga muziki wake katika miondoko ya Hip Hop.
Alisema katika tamasha hilo, wasanii hao wawili watatumbuiza mmoja mmoja na baadaye watatoa burudani kwa pamoja.
Koshuma aliongeza kwamba, kituo hicho kimekuwa na utaratibu wa kufanya maonesho ya utamaduni mara kwa mara, na wanawashukuru wadhamini wao Shirika la Ndege la Precision kwa kutoa usafiri kwa wasanii hao, ambao mara baada ya onesho la Dar es Salaam watakwenda Arusha Jumapili, kisha Kilwa ambako nako watafanya maonesho.
Chanzo: Tanzania Daima

Friday, November 16, 2012

Busara Promotions yaanda shindano la waandishi wa makala za mtandaoni na magazetini

Wandaaji wa tamasha la kila mwaka la Sauti za Busara, Busara Promotions wameandaa shindano la uandishi wa makala mbalimbali kuhusiana na tamasha hilo zitakazochapishwa mtandaoni na kwenye magazeti na washindi kuzawadiwa zawadi mbalimbali.
Katika taarifa yake kwa waandishi wa habari, Busara Promotions imeandika:
Hii ni stori kwa ajili ya waandishi, wachapishaji na wenye mitandao ya kijamii. Kitu pekee katika tamasha la kumi la Sauti za Busara ambalo litaanza tarehe 14- 17 Februari 2013. Tamasha limefikia muongo mmoja ambalo hakuna mfano wake. Waandishi wanaombwa kutuma makala mitandaoni, blog na wachapishaji wa magazeti.
Mbali na kushapisha na kuweka makala mbalimbali, makala bora na mwandishi/mtunzi bora atazawadiwa fulana ya tamasha, pasi ya bure ya siku zote za tamasha na Posho kama ishara ya shukrani. Tuma kupitia barua pepe hii press@busara.or.tz mwisho tarehe 30/11/2012.
Tunasubiria kupokea makala bora. Tutawapa idhini waandishi bora kuendelea kuweka makala zao, chapisho mbalimbali kwenye blogs na tovuti baada ya tarehe ya mwisho. Makala bora itajadiliwa kutokana na uhalisia, mtazamo na idadi ya mitazamo/maoni kutoka kwa wasomaji na mashabiki.
Kuhusu Sauti za Busara
Sauti za Busara hufanyika kila mwezi wa pili katika kisiwa cha marashi ya karafuu Zanzibar, tamasha hujulikana kama ‘Tamasha rafiki katika sayari ya Dunia’. Katika kuwawezesha wenyeji ili wafurahie tamasha bei ya tiketi kwa kila siku ni shilingi 3,000 kwa watanzania na wageni kutoka nchi za nje ni Dola 48 za kimarekani.
Tamasha la 10 litakutanisha vikundi mbalimbali kama ifuatavyo Cheikh Lô (Senegal) Mlimani Park Orchestra (Tanzania) Khaira Arby (Mali) Comrade Fatso and Chabvondoka (Zimbabwe) Culture Musical Club (Zanzibar / Tanzania) Atongo Zimba (Ghana / UK) N’Faly Kouyaté (Guinea) Nathalie Natiembe (Reunion) Zanzibar Unyago (Zanzibar / Tanzania) Nawal & Les Femmes de la Lune (Comoros / Mayotte) Wazimbo (Mozambique) The Moreira Project (Mozambique / South Africa) Owiny Sigoma Band (Kenya / UK) Mokoomba (Zimbabwe) Msafiri Zawose & Sauti Band (Tanzania) Mani Martin (Rwanda) Burkina Electric (Burkina Faso / USA) Lumumba Theatre Group(Tanzania) Sousou & Maher Cissoko (Senegal / Sweden) Super Maya Baikoko (Tanzania) Peter Msechu (Tanzania) Wakwetu Jazz Vibes (Tanzania) Safi Theatre Group (Tanzania) na wengineo.
Sauti za Busara hufanikiwa kuwaleta wageni wengi kila mwaka, lakini huifadhi misingi ya wenyeji. Hutoa fursa kwa wenyeji kuona na kusikiliza muziki kutoka sehemu mbalimbali za Afrika na vilevile kuutambulisha muziki wa Afrika Mashariki kwa wageni, fursa hii ni adhimu sana kiafya na kimaendeleo ya kimuziki.
Tamasha huwakutanisha watu pamoja kusheherekea na umoja, bila ya kuzingatia itikadi zao za kisiasa na kidini. Fursa kama hii ni adimu sana Zanzibar, na tukio hili limekuwa ni kiungo na muhimu katika kuimarisha umoja na amani, kujenga mahusiano mema na kuheshimiana.
Zaidi ya hayo, siku hizi watu wengi hutafuta mbinu muafaka za kujiwezesha kiuchumi kila, kupitia muziki na sanaa mbalimbali. Kwa matarajio yetu makubwa kabisa kwamba wageni huja kwa wingi na hutegemea kupata vitu adhimu kabisa kutoka kwetu, kama kufurahia muziki wakiwa na wenyeji wao.
Tamasha husaidia ukuwaji wa kiuchumi. Takwimu ya Serikali imeonyesha idadi ya wageni wanaokuja Zanzibar imeongezeka kwa zaidi ya asilimia 500 tangu lilipoanza tamasha.
Tamasha la Sauti za Busara hutoa mfano wa tukio ambalo lenye muundo wa kimaendeleo kwa pande zote wageni na wenyeji, kwa uthamini utajiri wa tamaduni mbalimbali za kiafrika. Huonyesha uzuri wa muziki wa tamaduni za kiafrika, na uwezekano wa kutengeneza ajira na kujiongezea kipato.

Song : Mr.Blue ft Man Walter – Nipende

Wednesday, October 17, 2012

AMTZ to establish online swahli course

Action Music Tanzania (Reg, No.BST 4733) has established Online Swahili lessons for any one who is interested to learn Swahili. The course aims at enabling a leaner to master how to listen, speak, write, and read Swahili language in a short time. There are many ways that we deliver our lesson including skype, you tube and our blog. Any one can choose time for the lesson to take part according to what she/he sees it fit. On the completion of the course you will be awarded with a certificate.
Though people have different reasons for learning Swahili, the most common interests in the language have been: its usefulness for research and travel purposes in East and Central Africa, meeting foreign language requirements in foreign academic institutions; and retracing the roots for the East African people living in Diaspora.
On other hand Swahili has been called a window for accessing East African culture. Many who have studied Swahili as a foreign language are continuously finding it useful in voluntary work and in the job market, especially among the many organizations that are getting involved in several projects in Africa. Many who go ahead to establish organizations working in East and Central Africa, either driven by social entrepreneurial goals or the traditional Aid Organizations, have also attested to its usefulness in penetrating the region.
Welcome and learn Swahili at affordable price. Karibu sana!
For fees structure, booking and scheduling your lesson please contact us by
actionmusictz@gmail.com establish